エピソード

  • CBC irekebishwe; Humphrey Obarah
    2022/08/27
    Katibu Mkuu wa Shirikisho la Talanta Duniani Profesa Humphrey Oborah, ambaye alivumbua kifaa cha kupima talanta na uwezo wa mwanafunzi kimasomo anaiataka serikali mpya kuifanyia sekta ya elimu nchini mageuzi ili kuhakikisha kuwa inaafikia malengo yake. Obarah anapendekeza Wizara ya Elimu kufanyiwa marekebisho na kuundwa kwa Wizara ya Masomo ambayo itahakikisha kuwa mageuzi yanafanyika katika sekta ya elimu nchini. Kwenye mazungumzo na Faith Kutere, Oborah aidha anapendekeza Mtaala wa Umilisi CBC kurekebishwa ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu bora.
    続きを読む 一部表示
    15 分
  • Wanafunzi pacha; alama sawa, KCPE na KCSE
    2022/04/28
    Brooke na Chelsea Sagala ni pacha ambao wamekuwa wakipata alama sawa au zinazokaribiana tangu walipoanza masomo. Wawili hawa walipata gredi ya B- ya alama 57 na kupata alama sawa kwenye masomo yote katika KCPE. Aidha, walipata alama sawa ya 380 kwenye mtihani wa KCPE. Faith Kutere amezungumza na pacha hawa ambao wanasema kuwa licha ya kutia bidii na kushindana masomoni, wamekuwa wakipata alama sawa. Wawili hawa wanalenga kujiunga na Chuo Kikuu cha Katoliki na kusomea uanasheria wakiwa na matumaini kuwa hawatatenganishwa na chochote maishani.
    続きを読む 一部表示
    14 分
  • Elimu ya kiufundi Ukraine; fursa za ajira ni chache - Paul Kurgat
    2022/03/03
    Paul Kurgat aliwahi kuwa Balozi wa Kenya nchini Ukraine na pia alisomea Ulaya, hasa Urusi. Kwenye Elimu Podcast, Balozi Kurgat anazungumza na Faith Kutere kuhusu elimu nchini humo na kulinganisha na mfumo wa elimu nchini Kenya. Pia anaeleza jinsi ambavyo vita kati ya Ukraine na Urusi vitakavyowaathiri wanafunzi wanaosomea huko.
    続きを読む 一部表示
    8 分
  • Elimu: Siku ya Kiswahili Duniani (UNESCO); tukitumie ofisini, siasani....
    2022/01/20
    Kiswahili ambacho ni lugha ya kitaifa na rasmi nchini Kenya kinazidi kupiga hatua duniani licha ya changamoto mbalimbali kuhusu matumizi yake nchini Kenya. Hatua kubwa zaidi katika maendeleo ya lugha hii ni kuhusu Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kuipa hadhi lugha hii kwa kutangaza Julai saba kila mwaka kuwa Siku ya Kiswahili Duniani. Mwaka wa 2021, magwiji na wakereketwa mbalimbali wa Kiswahili nchini Kenya wamezidisha sauti zao kuhusu haja ya Kiswahili kutumiwa katika mazingira rasmi kwani ni dhahiri kuwa Kiingereza kingali kupaumbele cha wengi katika maeneo ya kazi. Geoffrey Mung’ou ameandaa makala maalumu kuhusu hali ya Kiswahili, hatua zilizopigwa na yanayohitajika kufanywa ili kukabili changamoto kukihusu.
    続きを読む 一部表示
    24 分
  • Elimu Podcast; Baraza la Kiswahili; Prof. Kandagor Mosol-CHAKITA
    2021/11/13
    Harakati za kuhakikisha kuwa Kenya inakuwa Baraza la Kiswahili zimeshika kasi. Wizara ya Michezo na Utamaduni imeandaa warsha (tarehe 11 na 12 Novemba, 2021) jijini Nairobi na kuwashirikisha waandishi, wahadhiri na wawakilishi wa vyama vya Kiswahili kikiwamo CHAKITA, ili kujadili suala hili. Sikiliza podcast hii ambapo Geoffrey Mung'ou anamhoji Profesa Kandagor Mosol, Mwenyekiti wa CHAKITA vilevile mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Moi.
    続きを読む 一部表示
    20 分
  • Elimu Podcast: Mafadhaiko miongoni mwa vijana
    2021/10/17
    Mafadhaiko miongoni mwa vijana yameendelea kuwazonga na hata baadhi kukata tamaa maishani. Mwalimu Frank Otieno amezungumza kwa kina na washauri wa vijana: Evelyne Ogendo, Faith Mutendwa na Kelvin Ogada na kuangazia mbinu za kuwakwamua vijana kutokana na msongo wa mawazo nyumbani na hata shuleni.
    続きを読む 一部表示
    32 分
  • Elimu Podcast: TPD-Sh.6,000 kila mwaka; walimu waisuta TSC
    2021/10/03
    Tume ya Huduma kwa Walimu, TSC imetoa mwelekeo wa lazima kwa walimu wote kujiendeleza kitaaluma kupitia mpango uitwao Teacher Professional Development (TPD) utakaomgharimu kila mwalimu ada ya Sh.6,000/- kila mwaka. Mwalimu Frank Otieno anazungumza na Mwalimu Benitez Osukuku kuhusu suala hili.
    続きを読む 一部表示
    28 分
  • Elimu Podcast: Wanafunzi Wenye Mahitaji Spesheli
    2021/09/26
    Kenya inapochangamkia Mtalaa wa Umilisi (CBC), mwanafunzi mwenye mahitaji spesheli anashughulikiwaje?Mwalimu Frank Otieno amezumgumza na Daktari Festo Ndonye, ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Moi, Idara ya Elimu Spesheli na Eva Nabutuni, mwandishi wa kitabu cha kufunza walimu na wazazi kuhusu elimu ya wenye mahitaji spesheli.
    続きを読む 一部表示
    32 分