Kisa Changu

著者: The Standard Group PLC
  • サマリー

  • Watu mbalimbali wanasimulia wanayopitia ama kushuhudia kwa namna ya kugusa moyo, kushtua na kuliza machozi, vilevile kauli za matumaini.
    The Standard Group PLC
    続きを読む 一部表示
activate_samplebutton_t1
エピソード
  • Eliot Berry, Mwingereza anayependelea kuishi Kenya| Kisa Changu Podcast
    2022/11/27
    Eliot Berry, Raia wa Uingereza alikuja Kenya akiwa na umri wa miaka 19 alipotumwa na mamaye kutembea. Anasema alikuwa msumbufu na mara nyingi alikuwa akitoroka shuleni lakini alipofika Kenya alihisi kuwa nyumbani na maisha yake yakabadilika. Alianza rasmi kuishi nchini Kenya mwaka 2011 na amejifunza Kiswahili na pia Sheng kwa lengo la kutangamana na watu wa matabaka yote. Aidha, kwenye mitandao ya kijamii anakojulikana kama Reverend Dad, amekuwa akiwafurahisha watu kwa video za ucheshi kutumia Kiswahili. Katika Kicha Changu Podcast wiki hii tunaangazia maisha ya Reverend Dad, katika mahojaino haya na Faith Kutere.
    続きを読む 一部表示
    15 分
  • Familia zatafuta wapendwa wao, Mombasa | Kisa Changu Podcast
    2022/11/06
    Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa familia mbili kwenye eneo la Likoni katika Kaunti ya Mombasa zinaendelea kuhangaika kuwatafuta wapendwa wao ambao wanaaminika kuchukuliwa kwa nguvu na maafisa wa Idara ya Usalama. Tumesema na familia ya Bakari Mwanyota mwenye umri wa miaka 38 wa Mtaa wa Consolata na familia ya Tunu Said mwenye umri wa miaka 55. Familia hizo mbili zinasema wapendwa wao walichukuliwa kwa nguvu mwezi Februari na Julai, 2021 na hadi sasa hawajui waliko. Robert Menza amezungumza na familia za wawili hao katika makala haya ya Kisa Changu Podcast.
    続きを読む 一部表示
    20 分
  • Mlinzi wa Binafsi Aliyeponea Kifo | Kisa Changu Podcast
    2022/10/29
    Bernard Kibet amekuwa bawabu kwa zaidi ya miaka kumi. Japo kazi hii imemwezesha kuilisha familia yake na kuwasomesha watoto wake ni kazi ii hii ambayo imemsababishia machungu ambayo hatawahi kusahau kamwe. Kibet anasema wakati mmoja genge la majambazi lililokuwa kwenye eneo lake la kazi liliiba na kumpiga risasi kichwani bila kukusudia. Waliomwokoa walimchanganya na mili minane bila kukusudia tayari kupeleka katika hifadhi ya maiti lakini kwa bahati nzuri aliokolewa. Ilikuwa aje? Martin Ndiema amefanya mezungumzo na Kibet katika Podcast hii.
    続きを読む 一部表示
    12 分

あらすじ・解説

Watu mbalimbali wanasimulia wanayopitia ama kushuhudia kwa namna ya kugusa moyo, kushtua na kuliza machozi, vilevile kauli za matumaini.
The Standard Group PLC

Kisa Changuに寄せられたリスナーの声

カスタマーレビュー:以下のタブを選択することで、他のサイトのレビューをご覧になれます。